EMELDA MWAMANGA AWAHAMASISHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KUJIAMINI.








Akizungumza wakati wa semina ya wanawake wajasiriamali iliyoambatana na maonyesho ya bidhaa mbalimbali jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Afisa mtendaji mkuu wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Dare to Dream foundation iliyoandaa semina hiyo Emelda Mwamanga alisema  kutojiamini ni moja kati ya sababu zinazowafanya wanawake wajasiriamali kushindwa kusonga mbele




Emelda alisema kuwa, duniani ya sasa ya kibiashara imejaa ushindani mkubwa na bila kujiamini itakuwa ni vigumu kwa wanawake wajasiriamali kuweza kufanikiwa.


"Semina hii imewaleta pamoja wanawake wa kada mbalimbali ili kuweza kubadilishana uzoefu pamoja na kutiana moyo. Wapo waliofanikiwa kibiashara ambao watawaeleza wale ambao bado hawajafanikia njia walizopitia mpaka kufika hapo walipo. Kupitia semina hii watajifunza na namna ya kutengeneza bidhaa zenye viwango pamoja na namna ya kujitanga," alisema



Kwa upande wake Afisa masoko wa benki ya CRDB Emmanuel Kiondo alisema kuwa benki yake inatambua umuhimu wa kumwezesha mwanamke na ndiyo maana ikaamua kujitokeza kudhamini shughuli hiyo iliyolenga kuwajengea uwezo wanawake 



Tunaamini kuwa mwanamke akiwezeshwa familia nzima inakuwa imewezeshwa. Benki ya CRDB imekuwa ikimjali sana mwanamke na tumeweza kuanzisha akaunti ya Malkia maalumu kwa ajili ya wanawake wenye malengo mbalimbali ikiwemo ya kiujasiriamali," alieleza



Mwakilishi kutoka kampuni ya Vodacom ambao ndiyo wadhamini wakuu wa semina na maonyesho hayo Alice Lewis alisema Vodacom inatambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii na itaendelea kuwa mstari wa mbele kuwasaidia kusonga mbele.






0 comments:

Copyright © 2013 Owned and Managed by Bouner Disneysorata Tanzanite! All right Reserved..