WENYE MSIMAMO
Wanawake daraja la kwanza wanaopendwa zaidi na wanaume ni wale wenye msimamo, uelewa mkubwa wa mambo na maamuzi sahihi, wako makini kwenye matendo yao na siku zote hufanya vitu kwa ajili ya kupata mafanikio.
WAPENDA USAWA
Aina ya pili inayohitajika katika katika ulimwengu wa kimapenzi ni wanawake wanaoheshimu usawa wa jinsia, walio tayari kubeba majukumu ya kifamilia kwa ulinganifu sawa na wanaume, wenye uwezo wa kuongoza jamii kwa asilimia 50 kwa 50.
WANAOJUA MAPENZI
Wanawake wajuzi wa mambo ya faragha wanapendwa sana. Sifa yao kubwa ni uwezo wa kutosheleza katika tendo la ndoa. Tafiti zinaonyesha kuwa wanaume hupenda sana wanawake watundu katika mchezo wa sita kwa sita. Mara nyingi wanatajwa kuwa na uwezo wa kuteka akili za wanaume bila kujali sifa zao za nje au za ndani.
MARAFIKI
Wanawake wenye sifa sawa na rafiki ni aina ya nne inayowavutia wanaume. Wao hutegemea zaidi nguvu ya kushawishi inayotokana na namna wanavyojali na kujitolea kuhakikisha wanakuwa marafiki wa kweli kwenye shida na raha kwa wapenzi wao. Si wakorofi, waungwana na wapenda amani.
WA WAZI
Aina nyingine ya wanawake inayowavutia wanaume ni wenye msimamo na uwazi. Si wepesi wa kuburuzwa katika maamuzi ya msingi kwa kisingizio cha wao ni wanawake. Utafiti unaonesha wanawake wa aina hii wamekuwa muhimu hasa kwa wanaume wenye tabia za ubabe na udhaifu katika uelewa wa mambo.
WANAOJITEGEMEA
Wanawake wanaojitegemea wana soko kubwa kwa wanaume tofauti na akina naomba vocha kila siku. Uchunguzi unaonyesha kuwa wanaume wa leo hawapendi wanawake tegemezi, wasiokuwa na kazi na wanaoendekeza starehe za upande mmoja.
WASIO NA PRESHA
Nikisema wanawake wasiokuwa na presha namaanisha wasiolazimisha vitu vitokee haraka haraka. Wao siku zote huacha mambo yatokee yenyewe na kazi yao kuwa ni kutenda sehemu ya majukumu yao kama wapenzi.
MARIDADI
Kundi lingine la wanawake wanaopendwa na wanaume ni wanaozingatia usafi na kujiremba. Wanaokwenda na wakati katika mavazi na mvuto wa nje. Lakini pia ni welewa wa mazingira, si wasamba. Wanapendeza kwa muonekano.
WANAORIDHIKA
Wanawake ambao hulidhika na hali walizonazo ni kivutio kikubwa kwa wanaume, hili ni kundi linalohitajika sana katika ulimwengu wa mapenzi kwa upande wa wanaume ambao maisha ya sasa yamekuwa yakiwageuza kutoka juu kwenda chini au chini juu. Kukubali hali zote bila kubadili tabia ni sifa njema ya mwanamke.
WA MMOJA
Wanawake wanaochagua mara moja na kutosheka na kuwa tayari kukwepa kila aina ya vishawishi toka kwa wanaume ambao kimtazamo wana vitu vya ziada zaidi ya waliowachagua mwanzo wanahitajika sana. “Niliye naye ananitosheleza kwa kila kitu sitaki mtu mwingine.” Kundi la wanawake wa aina hii ni adimu na muhimu sana.
Kwa hisani ya jitambue
Fedha: Katika swala la fedha, jambo kubwa linalojitokeza ni namna ya kufanya maamuzi kuhusu matumizi ya fedha. Ni muhimu kuweka mikakati ya pamoja kwa mambo ya msingi kimaisha , na kila mmoja kutilia maanani mipango hiyo, kabla ya kuamua kutumia kipato chake kwa mambo ambayo pengine hayapo nje ya mipango ya kifedha ya wawili nyie kama wapenzi. Bila shaka, kuendana na aina yenu ya kipato, aina yenu ya maisha, kama wapenzi mtakuwa na kiwango fulani cha fedha ambacho si busara mmoja wenu kuamua kutumia bila kumtaarifu mwenzake , hata kama matumizi husika ni muhimu sana, na haijalishi nani kazitafuta fedha husika.
Imani: Katika swala la imani, ni muhimu
kufahamiana vema mwenendo wa kiimani wa mwenza wako, na kuheshimu kuwa swala
hili ni nyeti, na mabadiliko ya kweli hayawezi kulazimishwa. Imani inaweza
athiri namna mnavyoweza kuwasiliana kama wapenzi – kwani mwingine mwenye
msimamo mkali wa kidini, anaweza kukataa jambo fulani hapo baadae, jambo ambalo
pengine mwenza wake anaona ni jambo la kawaida tuu. Imani inaathiri malezi ya
watoto, na inaweza athiri shughuli za kiuchumi za wawili nyie, mfano pale mmoja
wenu anapoamua kujikita katika ‘huduma’
zaidi, kuliko familia na shughuli za kuingiza kipato.
Mahali pa kuishi: Mtaa gani , wilaya gani, mkoani gani, nchi
gani au bara gani kila mmoja wenu anatazamia muishi ni jambo la msingi kuliweka
wazi kati yenu. Jambo hili linaweza kuendana na mambo mengine mengi ambayo
yanachochea mabadiliko ya muda mfupi na hata muda mrefu katika maisha yenu,
kama vile , aina ya kazi mnazotarajia kila mmoja wenu kufanya, na aina ya kazi
unazotamani au kufikiri ni vema mwenza wako afanye.
Watoto: Hili ni jambo zito haswa katika
vipengele vya lini watoto wapatikane (ujauzito), idadi ya watoto, aina ya
malezi kwa watoto watakaopatikana, na zaidi sana majukumu ya kifedha katika
malezi ya watoto (mfano, nani atalipa ada ya shule, n.k). Pamoja na kutafakari
hayo, watu wawili mlio katika mahusiano, ni muhimu mkatengeneza picha ya maisha
ya watoto wenu endapo mmoja wenu atatangulia mbele za haki (atafariki), na hata
ikiwezekana mwaweza fikiria na kupanga
aina ya maisha mnayotaka watoto wenu waishi pale nyote wawili hamtokuwepo duniani. Inapotokea mambo kama hayo
yaliyotajwa hapo juu hayajawekwa wazi mbele yenu, ni rahisi mmoja wenu kufanya
mambo yasiyompendeza mwengine –mfano wakati mwingine anafikiria akiba ya baadae
ya watoto ili wakasome international school, mwingine anafikiria namna ya
kutanua ili ‘kuuza sura’.
Falsafa ya maisha: Swala hili linahusu wa kipekee na tafakari
huru ya kila mmoja wenu kuhusu mambo kadhaa ya kimaisha kama vile mtazamo wa
kila mmoja wenu kuhusu biashara (mwingine biashara ni kitu cha kuweka heshima
kwa jamii, wakati mwingine biashara ni kielelezo cha huduma kwa jamii na hivyo
kinahitaji muendelezo).
Falsafa
pia inahusu namna kila mmoja wenu anavyochukulia mambo kama vile kusaidia watu
wengine, kuwa na mahusiano na watu wa
jinsia tofauti (wapo wasiotaka hata classmet ampigie simu mpenzi wake). Falsafa
pia inahusika na namna kila mmoja anavyotafsiri mafanikio katika maisha, na alivyo
tayari kufanya yanayopaswa kufanywa kufikia mafanikio (Mfano, wengine mafanikio
ni mali na umaarufu, wakati kwa wengine mafanikio ni namna anavyoweza kuwa na
furaha na uhuru , pamoja na kusaidia wengine).
Katika
juhudi za kufikia mafanikio unawea kukuta wapenzi mnatofautiana kwani mmoja
anaweza amini rushwa ndio suluhisho pekee la kufikia anakotaka, wakati mwingine
anaamini tofauti na hivyo.
Hisia za kimapenzi: Ni jambo la msingi
kutokupuuzia hisia za kimapenzi za kila mmoja wenu. Tambua vile mwenzako
angependa akuone unamvutia na vile ambavyo unamjali hisia zake. Ni kweli kuwa
katika mahusiano, hisia za kimapenzi zinaweza zisichukue nafasi kubwa kati yenu
kwani kuna mambo mengi ya kufanya pamoja kama wapenzi, hata hivyo pamoja na
udogo wake wa muda, jambo hili nyeti lisipopewa kipaumbele, linaweza sababisha
mengine yote kuharibika. Zaidi sana, kumbuka wewe na mpenzi wako, ni watu wa
jinsia mbili tofauti, kinachowafanya muungane kiasili ni hizo hisia za mapenzi
kati yenu.
Hitimisho: Sio lazima kama watu wawili
mlio katika mahusiano muwe na mtazamo sawa katika hayo yote yaliyoelezwa hapo
juu, hata hivyo, ni muhimu sana kwenu nyote kuwa na picha kichwani ya mtazamo
wa mwenza wako kuhusu mambo hayo niliyotaja hapo juu.
Pale
mnapokubaliana kutofautiana katika
mambo yaliyotajwa hapo juu (mf.mambo ya fedha, na imani), hakikisheni mnakubaliana bila
kutofautiana kuhusu athari za kutofautiana kwenu, na jukumu la kukubali
athari hizo kwa mahusiano yenu.
Hizi hapa sababu toka kwa,
Dokta Bianca P. Acevedo kutoka Chuo Kikuu cha California, Santa Barbara anasema, wanawake huchangia kwa kiasi kikubwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume,kwa haya yafuatayo;
1: KAULI
Miongoni mwa mambo ambayo mwanaume hataki kuyasikia yakitoka kwenye kinywa cha mwanamke ni kuambiwa HAWEZI TENDO LA NDOA. Mwanamke akimwambia mwanaume wakati au baada ya tendo kuwa hawezi, atakuwa amemsababishia tatizo kubwa la kisaikolojia ambalo litampelekea kupotea nguvu za kiume taratibu.
Msaada unaohitajika kwa mwanamke anayekutana na mwanaume dhaifu kwenye tendo si kumwambia hawezi, bali ni kumtia moyo na kumsaidia kuweza. Wanawake wamewasababishia waume zao upungufu wa nguvu za kiume kwa kuwaambia maneno kama haya: “Yaani siku hizi sijui umekuwaje, yaani huwezi kazi kabisa!”
2 : UJUZI
Wanawake wengi hasa waliopo kwenye ndoa, wanapuuza ujuzi kwenye tendo la ndoa. Hawajishughulishi kumsaidia mwanaume ‘kuwika’, si wabunifu na watundu, jambo hili humfanya mwanaume kushiriki tendo kwa kutegemea kupanda kwa hisia zake mwenyewe, hivyo anapokuwa amechoka au ana mawazo, hawezi kusisimka kwa vile hapati ushirikiano toka kwa mwenzake.
Pamoja na wengi kutokuwa wajuzi, lakini wapo wengine ambao ni watundu mno kwenye sita kwa sita kiasi cha kumfanya mwanaume ajione kama mgeni wa mchezo huo.
Kimtazamo, wanaume hupenda sana ushindi wakati wa ‘kazi’, lakini pale wanapogeuzwa ‘chekechea’ hupunguza uwezo wa kujiamini na kuruhusu hofu kuongezeka mawazoni mwao, hivyo kuwasababishia tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Inashauriwa kwamba, mwanamke anapokuwa na uelewa mkubwa wa masuala ya mapenzi hasa wakati wa tendo, asioneshe kiwango kikubwa kwa haraka bali amchukulie mwenzake kama mwanafunzi, asiwe na maneno kama: “Leo nakuja kukupa vitu adimu kuliko vya juzi, hakuna kulala kasi mtindo mmoja.” Kauli hizi huwaogopesha wanaume na kuwafanya wapungukiwe na nguvu.
USAFI
Mwanamke anapokuwa si msafi, huweza kumsababishia mwanaume matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume. Sote tunafahamu umuhimu wa usafi wa mwili na kero za uchafu wakati wa tendo, hivyo ni wazi kuwa mwanamke akiwa mchafu atamfanya mwanaume apoteze msisimko na uwezo wa tendo la ndoa. Unadhifu wa mavazi na mwili ni muhimu sana katika mapenzi.
GUBU
Jambo lingine linaloweza kumsababishia mwanaume upungufu wa nguvu za kiume ni gubu au karaha za maneno ya uchokozi yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Uchokonozi wa mambo, ugomvi, usaliti na hali ya kutokuwa na staha ni mambo yanayosababisha tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Mwanamke anapokuwa mwingi wa maneno ya kashfa, dharau na matusi huweza kumfanya mume amchukie na kutopenda kushiriki naye tendo. Uchunguzi unaonesha kwamba wanawake walioolewa wenye tabia hii, huwafanya waume zao wawe na msisimko wa kimapenzi kwa wanawake wa nje kuliko wake zao hao.
USALITI
Tabia ya usaliti kwa mwanamke ni chanzo kingine cha mwanaume kupata tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Mwanaume anapoona, kuhisi au kubaini kuwa anasalitiwa, huumia sana moyoni, maumivu ambayo hatimaye humfanya muhusika kuwa na mawazo mengi ambayo humuondolea hamu ya tendo.
Kwa hisani ya chimbuko letu.
Subscribe to:
Posts (Atom)